Tuesday 29, Jul 2025

728x90 AdSpace

­
Latest News
    September 1, 2014

    USAJILI: Chicharito Ajiunga na Real Madrid kwa Mkopo.


    Akiwa na jezi yake mpya ya Real Madrid na Rais wa klabu hiyo Perez
    Wakati akichukuliwa vipimo vya afya na kubainika yupo fiti
    Akiangunga saini ya kuichezea klabu hiyo bingwa ya Ulaya
    MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Mexico, Javier Harnendez Chicharito amefaulu vipimo vya kujiunga na klabu ya Real Madrid na amekabidhiwa jezi namba 14 kwa ajili ya kuichezea wababe hao wa Ulaya kwa mkopo akitokea klabu yake ya Manchester United.

    Chichirito ambaye hakuwa na nafasi katika kikosi cha kwanza cha Mashetani Wekundu tangu alipotua akitokea kwao Mexico, amejiunga na Madrid akimpisha Ramadel Falcao aliyetokea Monaco aliyetua Old Trafford kwa mkopo vilevile.
    Mshambuliaji huyo alitua Old Trafford mnamo mwaka 2010 na amenyakuliwa na Madrid ili kuchukua nafasi ya Alvaro Morata ambaye aliuzwa Juventus.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 blogger-facebook:

    Post a Comment

    Item Reviewed: USAJILI: Chicharito Ajiunga na Real Madrid kwa Mkopo. Rating: 5 Reviewed By: Unknown