728x90 AdSpace

­
Latest News
March 10, 2017

Zijue Mbinu za kukusaidia Kuwa Mbunifu Kwenye Biashara


Na. James Waibina.
Karibu Mpenzi Msomaji na mfuatiliaji wa Makala zetu katika Blog hii ya Fumbuka..
Leo katika Makala hii ya "Fursa kwa wote" ninakuletea njia zitakazo kusaidia ili uweze kuwa mbunifu katika biashara yako, tambua kuwa biashara ili ikue inahitaji ubunifu utakaokusaidia kubuni mbinu mbalimbali na kuhakikisha biashara yako inakuwa na mafanikio makubwa.

Yafuatayo ni mambo ya kufanya ili uweze kuwa mbunifu, karibu tuwe sote...

    1.  Jenga Urafiki na Watu
Kuwa na urafiki na watu ambao wamefanikiwa kwenye biashara kama yako ni njia mojawapo ya kukusaidia kuwa mbunifu.
Ukiwa na ukaribu na watu ambao wanafanya biashara kama yako na wamefanikiwa utajifunza mambo mengi sana kutoka kwao, pale ambapo wewe ulikuwa unakosea utajifunza na pale ambapo ulikuwa sio bora utaumiza kichwa kubuni kitu kipya ambacho kitakufanya kuwa bora zaidi.

    2.  Jisomee Vitabu na Majarida.
Tafuta vitabu vya watu waliofanikiwa kwenye biashara ambayo wewe unataka kuifanya, vitabu vimeeleza siri mbalimbali zitakazokufanya kuwa mbunifu kwenye biashara yako, jitahidi sana kuwa msomaji wa vitabu mbalimbali vinavyofundisha biashara kama unayofanya vitakujengea uwezo mkubwa sana wa kuwa mbunifu kwenye biashara yako.

Vitabu vitakupa mbinu mbalimbali za kufanikiwa kwenye biashara yako, kumbuka vitabu havipatikani bure lazima ununue kwahiyo hakikisha unanunua vitabu na unavisoma ili uweze kuongeza maarifa zaidi.

    3.  Hudhuria Semina na Makongamano.
Watu wengi hawapendi kuhudhuria semina na makongamano ya ujasiriamali lakini ngoja nikwambie kitu kama unataka kufanikiwa kwenye maisha yako hakikisha unatafuta semina nyingi sana hata kwa kulipia nenda kalipie ukajifunze utapata mawazo mengi sana ambayo yatakusaidia kuwa mbunifu kwenye biashara yako, kwasababu utakuwa kila siku unapata mawazo mapya utajikuta kila siku unajua njia za kuboresha biashara zako na hapo ndipo ubunifu huzaliwa, lakini kama unafikiria ukianzisha tu biashara ndio basi, utafeli sana kwenye biashara zako.

    4. Kuwa na Mentor
Mentor ni Mlezi Mshauri, hakikisha una mlezi kwenye biashara yako, kama hauna mlezi ni kazi sana kufanikiwa kwenye biashara tafuta mentor ambae atakuwa anakuongoza kwenye biashara yako, huyo anakuwa anakupa mawazo mapya na ushauri wa kufanikiwa kwenye biashara yako,utafanikiwa sana na utakuwa mbunifu.

Hizo ndio njia pekee unazoweza kuzitumia kuwa mbunifu.

Ahsante.
Kwa Maoni /Ushauri: Tuwasiliane kupitia

0713515059  -(WhatsApp) au  jameswaibina@fumbuka.co.tz
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 blogger-facebook:

Post a Comment

Item Reviewed: Zijue Mbinu za kukusaidia Kuwa Mbunifu Kwenye Biashara Rating: 5 Reviewed By: Unknown