728x90 AdSpace

­
Latest News
March 13, 2017

MASOMO YA MISA: Dominika ya 2 ya Kwaresima Mwaka A, Tarehe 12/03/2017


MWANZO:
Zab. 27:8 – 9

Moyo wangu umekuambia, Bwana, uso wako nitautafuta. Usinifiche uso wako.

SOMO 1
Mwa. 12:1 – 4a

Bwana akamwambia Abrahamu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha; nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulitukuza jina lako; nawe uwe Baraka; nami nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani; na katika wewe jamaa zote za dunia watabarikiwa.
Basi Abramu akaenda, kama Bwana alivyomwamuru.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI
Zab. 33:4 – 5, 18 – 20, 22 (K) 22

(K) Ee Bwana, fadhili zako zikae nasi, Kama vile tulivyokungoja Wewe.

Kwa kuwa neno la Bwana lina adili,
Na kazi yake yote huitenda kwa uaminifu.
Huzipenda haki na hukumu,
Nchi imejaa fadhili za Bwana. (K)

Tazama, jicho la Bwana li kwao wamchao,
Wazingojeao fadhili zake.
Yeye huwaponya nafsi zao na mauti,
Na kuwahuisha wakati wa njaa. (K)

Nafsi zetu zinamngoja Bwana;
Yeye ndiye msaada wetu na ngao yetu.
Ee Bwana, fadhili zako zikae nasi,
Kama vile tulivyokungoja Wewe. (K)

SOMO 2
2Tim. 1:8b – 10

Uvumilie mabaya pamoja nami kwa ajili ya Injili, kwa kadiri ya nguvu ya Mungu; ambaye alituokoa akatuita kwa mwito mtakatifu, si kwa kadiri ya matendo yetu sisi, bali kwa kadiri ya makusudi yake yeye na neema yake. Neema hiyo tulipewa katika Kristo Yesu tangu milele, na sasa inadhihirishwa kwa kufunuliwa kwake Mwokozi wetu Kristo Yesu; aliyebatili mauti, na kuufunua uzima na kutokuharibika, kwa ile Injili.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

SHANGILIO
Mt. 17:5

Sauti ya Baba ilitoka katika wingu jeupe: “Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, msikieni yeye.”

INJILI
Mt. 17:1 – 9

Yesu akawatwaa Petro, na Yakobo, na Yohane nduguye, akawaleta juu yam lima mrefu faraghani; akageuka sura yake mbele yao; uso wake ukang’aa kama jua, mavazi yake yakawa meupe kama nuru. Na tazama, wakatokewa na Musa na Eliya, wakizungumza naye.
Petro akajibu akamwambia Yesu, Bwana, ni vizuri sisi kuwapo hapa; ukitaka, nitafanya hapa vibanda vitatu, kimoja chako wewe, na kimoja cha Musa, na kimoja cha Eliya.
Alipokuwa katika kusema, tazama, wingu jeupe likawatia uvuli; na tazama, sauti ikatoka katika lile wingu, ikasema, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye; msikieni yeye. Na wale wanafunzi waliposikia, walianguka kifulifuli, wakaogopa sana.
Yesu akaja, akawagusa, akasema, Inukeni, wala msiogope. Wakainua macho mlimani, Yesu aliwaagiza, akasema, Msimwambie mtu yeyote habari ya maono hayo, hata Mwana wa Adamu atakapofufuka katika wafu.


Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 blogger-facebook:

Post a Comment

Item Reviewed: MASOMO YA MISA: Dominika ya 2 ya Kwaresima Mwaka A, Tarehe 12/03/2017 Rating: 5 Reviewed By: Unknown