728x90 AdSpace

­
Latest News
September 7, 2014

UKAWA WATOLEWA NJE KUKUTANA RAIS WA ZANZIBAR

 
Zanzibar. Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein ametupilia mbali maombi ya kumtaka kufungua mazungumzo na viongozi wa Ukawa, ili kupatikana kwa mwafaka kwa wabunge wa Bunge la Katiba kutoka Zanzibar na kurejea bungeni.

Akizungumza na Mwananchi Katibu wa Kamati ya Kuwaunganisha wabunge kutoka Zanzibar, Mohamed Yussuf Mshamba amesema kamati yake imepokea barua maalumu kutoka Ofisi ya Rais ikiwataarifu kuwa Rais hayuko tayari kufungua mazungumzo hayo.

“Tumepokea majibu kutoka Ofisi ya Rais, Ikulu Zanzibar, tumeelezwa kuwa suala hilo ni vyema likabaki mikononi mwa Bunge la Katiba na suala la usuluhishi imeshauriwa tufanye wenyewe ZIRPP,” alisema Mshamba.


Aidha alisema kwamba kutokana na msimamo huo wa Rais Dk Shein, kazi ya kuwaunganisha wabunge wa Zanzibar imekuwa ngumu kwa vile matarajio ya ZIRPP ilitegemea kazi hiyo ingerahisishwa na Rais na kuzika tofauti ya kimsimamo.

Mshamba alisema maombi yao waliyawasilisha Agosti mwaka huu baada ya kamati ya kuwaunganisha Wazanzibari kukamilisha kazi ya kukusanya maoni ya wananchi kupitia kongamano la wazi juu ya nini kifanyike na kuhakikiisha Wazanzibari wanamaliza tofauti zao na kutetea maslahi ya Zanzibar.

‘Kwa ufupi kazi ambayo tumekuwa tukijaribu kuifanya imekuwa ngumu, tunachowaomba wabunge wa Zanzibar waache tofauti za kiitikadi na kuweka mbele maslahi ya Zanzibar, njia pekee rahisi na mwafaka warudi bungeni kushirikivikao,” alisisitiza Mshamba.

Alisema kimsingi kuna makosa yaliyofanyika tokea mwanzo, ikiwa ni pamoja na utungaji wa sheria yenyewe ya Bunge la Katiba na kujikuta wakiingizwa wanasiasa kwenye Bunge hilo, badala ya kuwa la wataalamu na watu wengine wasiotokana na vyama vya kisiasa.

Mshamba alieleza kuwa kuanza kwa ‘mguu’ huo mbaya kumesababisha kuzuka kwa mivutano na mijadala yenye mitazamozaidi ya itikadi za kisiasa badala ya kuongozwa na nguvu ya hoja, ufahamu, upembuzi yakinifu na uzoefu wa wabunge wa Bunge hilo.


“Chadema pekee ndicho ambacho katika ilani yake iliahidi kuwa kikishika madaraka ya uongozi kitabeba jukumu la kuandika katiba mpya, si CCM, NCCR-Mageuzi, TLP wala CUF vilivyoahidi jambo hilo, sasa inashangaza kuona vyama hivyo vimekuwa mstari wa mbele kushupalia Katiba Mpya na kususia Bunge la Katiba,” alisema Mshamba.



Source: MWANANCHI
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 blogger-facebook:

Post a Comment

Item Reviewed: UKAWA WATOLEWA NJE KUKUTANA RAIS WA ZANZIBAR Rating: 5 Reviewed By: Unknown