728x90 AdSpace

­
Latest News
August 18, 2014

SHIBUDA AJITOA CHADEMA.. Anena Kutogombea Ubunge kupitia chama Hicho.

[Image: 1.jpg]
MBUNGE wa Maswa Magharibi, John Shibuda (Chadema), amesema hatagombea ubunge kupitia Chadema katika Uchaguzi Mkuu ujao, kwa kuwa amechoshwa na kauli za vitisho na kejeli dhidi yake, zinazotolewa na baadhi ya viongozi wa juu wa chama hicho.

Amesema hayo jana kwa nyakati tofauti, wakati akizungumza na wazee wa Mji wa Maswa na Malampaka wilayani humo, alipokuwa akijibu swali lao kuhusu hatima yake ya kisiasa ndani ya Chadema, baada ya chama hicho kutishia kumfukuza.

Alipoulizwa na wazee ni chama kipi atagombea ubunge katika Uchaguzi Mkuu ujao, alisema wakati ukifika atasema kwani kwa sasa bado anatimiza wajibu wake wa kutetea wapiga kura wake ambao wengi wao ni wakulima na wafugaji na yuko tayari kufukuzwa ndani ya Chadema kwa kuwatetea wao.

Alisema kuwa aliingia katika chama hicho kwa hiari yake baada ya kukataa dhuluma alizodai kufanyiwa na CCM na kudhani ndani ya Chadema kuna demokrasia na ukombozi wa kweli, lakini alichokikuta ni tofauti kwani kila siku amekuwa akipata misukosuko kutoka ndani ya chama hicho.

"Mie niliingia Chadema kwa hiari yangu baada ya kuona dhuluma zilizokuwa ndani ya CCM, chama kilichonilea kisiasa, nikaona heri niende Chadema ambako nilidhani kuna demokrasia na ukombozi wa kweli, lakini nilichokikuta humo ni tofauti kwani kila siku wazee wangu mnasikia napata misukosuko isiyo na maana," alisema.

Alisema pamoja na misukosuko hiyo, amekuwa kimya muda mrefu kiasi kwamba kuna wakati vijana ndani ya chama hicho walimtukana matusi, wakatoa maneno mbalimbali ya kumdhalilisha kwa kumwita ‘Msaliti’ na ‘Pandikizi wa CCM’, huku viongozi wa ngazi za juu wa chama hicho, wakikaa kimya bila kuchukua hatua.

"Pamoja na shutuma zote zinazotolewa juu yangu na kupachikwa majina mbalimbali kuwa mie ni ‘Msaliti’ mara ni ‘Pandikizi la CCM’, lakini hata siku moja sijawahi kuitwa katika Kamati Kuu ya Chadema na kuhojiwa.
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 blogger-facebook:

Post a Comment

Item Reviewed: SHIBUDA AJITOA CHADEMA.. Anena Kutogombea Ubunge kupitia chama Hicho. Rating: 5 Reviewed By: Unknown