728x90 AdSpace

­
Latest News
August 25, 2014

MWANAFUNZI WA DARASA LA SABA ABAKWA NA MUUZA GENGE




Kwenye Kituo cha Polisi cha Maturubai kilichopo Mbagala, Dar kuna faili la kesi namba MBL/RB/ 9817/2014- KUFANYA MAPENZI NA MWANAFUNZI ambalo linamsaka kijana Juma Athumani (30), mkazi wa Charambe, Mbagala kwa kosa la ubakaji wa denti wa darasa la saba.

Habari za kiintelijensia zilidai kwamba mtuhumiwa huyo ambaye ni muuza genge, alitenda kosa hilo Agosti, mwaka huu ambapo denti huyo alikuwa ametumwa na mama yake gengeni.
 
Ilisemekana kwamba jamaa huyo alimuomba denti huyo wazungumze kidogo ndipo akampeleka gesti kwa lazima.

Akizungumza na mwandishi, denti huyo alisema kuwa alipofika gesti, jamaa huyo alilipa fasta na kumvutia chumbani ambapo alianza kumshika ‘manido’ kisha akamtupia kitandani na kumwingilia kimwili bila ridhaa yake.

Alisema kwamba, jamaa alipomaliza shida zake, alimpa buku tano (5,000/=) lakini alipokataa huku akilia ndipo mwanaume huyo akamuongezea hadi ikafika buku kumi (10,000/=).
 

“Niliporudi nyumbani mama aliniuliza kwa nini nimechelewa kisha akaziona hela, akaniuliza nimezipata wapi, nikamwambia amenipa Juma ndiyo tukaenda hadi gengeni kwa Juma kuuliza ndiyo mama akagundua kuwa nimebakwa.

“Baadaye mama alikwenda kuripoti polisi ndipo Juma akakamatwa na mimi nikapelekwa hospitali na kugundulika kweli nilikuwa nimebakwa,” alisema denti huyo.
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 blogger-facebook:

Post a Comment

Item Reviewed: MWANAFUNZI WA DARASA LA SABA ABAKWA NA MUUZA GENGE Rating: 5 Reviewed By: Unknown