728x90 AdSpace

­
Latest News
July 18, 2014

AJALI YA NDEGE YA MALAYSIA YAUA ZAIDI YA WATU 280,Tazama ilivyoteketea baada ya Kudondoka

Ndege ya Malaysia, Boeing 777 iliyokuwa inatoka Amsterdam kwenda Kula Lumpur imeanguka Mashariki mwa Ukraine karibu kabisa na mpaka wa Russia, leo, July 17,2014.


Kwa mujibu wa CNN, waziri wa Malaysia anaehusika na mauala ya Usafirishaji amesema kuwa abiria 280 na wafanyakazi 15 waliokuwa kwenye ndege hiyo wamepoteza maisha.

Tweet ya Malaysia Airlines imeeleza kuwa ndege hiyo ilipoteza mawasiliano baada ya kutoka Amsterdam.

Kumekuwa na taarifa za awali kuwa ndege hiyo ilipigwa na  Ukraine, taarifa ambazo zimekanushwa na Raisi wa Ukraine.

Rais wa Malaysia ameeleza kupitia twitter jinsi alivyosikitishwa na tukio hilo na kudai kuwa wataanza uchunguzi wa tukio hilo haraka iwezekanavyo kufahamu chanzo.

Tukio hili linatokea wakati ambapo bado ndege ya nchi hiyo, Flight 370 iliyopotea March 8, Mwaka huu bado haijapatikana.

Miili kadhaa ya watu imesambaa katika eneo ilipoanguka ndege hiyo karibu na kijiji cha Grabovo, kinachodaiwa kushikiliwa na waasi.

Hivi ndivyo Ndege ya Malaysia ilivyoteketea baada ya kudondoka na kuyachukua maisha ya wote waliokuwepo ndani yake (watu 280)
Ndege hiyo ya MH17 ilikuwa inakaribia kuingia katika ardhi ya Urusi wakati ilipopoteza mawasiliano.
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 blogger-facebook:

Post a Comment

Item Reviewed: AJALI YA NDEGE YA MALAYSIA YAUA ZAIDI YA WATU 280,Tazama ilivyoteketea baada ya Kudondoka Rating: 5 Reviewed By: Unknown